Upatikanaji viungo

Breaking News
Jumapili, Aprili 27, 2025 Local time: 03:23

Mtu anayeaminika kuwa na umri mkubwa zaidi duniani afariki Ufaransa


Picha ya mtawa Lucile Randon au Sister Andre akiwa kwenye mji wa Toulon, kusini mwa Ufaransa mwaka uliopita.
Picha ya mtawa Lucile Randon au Sister Andre akiwa kwenye mji wa Toulon, kusini mwa Ufaransa mwaka uliopita.

Mtawa kutoka Ufaransa anayeaminika kuwa mtu mwenye umri mkubwa zaidi duniani ameaga dunia wiki chache kabla ya kusherehekea miaka  119 tangu kuzaliwa, kwa mujibu wa ripoti iliyotolewa na msemaji wa kituo cha afya  Jumatano kusini mwa Ufaransa.

Lucile Randon ambaye pia anajulikana kama sister Andre alizaliwa kwenye mji wa Alews kuisini mwa Ufaransa Februari 11, 1904. Msemaji huyo kwa jina David Tavella amesema pia kwamba Andre ni manusura mkongwe zaidi wa maambukizi ya covid-19 na kwamba amefariki Jumanne akiwa kwenye kituo cha afya cha St Catherine Laboure kilichoko kwenye mji wa Toulon.

Kundi la utafiti la Gerontology ambalo huorodhesha watu wenye umri wa zaidi ya miaka 110 au zaidi limeorodhesha Sister Andra kama mtu mwenye umri mkubwa zaidi ulimwenguni baada ya kifo cha Kane Tanaka kutoka Japan mwaka uliopita akiwa na umri wa miaka 119.

XS
SM
MD
LG