Upatikanaji viungo

Breaking News
Jumapili, Februari 09, 2025 Local time: 11:59

Mtoto wa rais wa Equatorial Guinea achunguzwa


Mtoto wa kiume wa  rais wa muda mrefu wa Equatorial Guinea anachunguzwa kuhusiabna na  madai ya utekaji na mateso.

Wadadisi wanasema madai hayo yataharibu juhudi za rais huyo kuboresha sifa yake kimataifa.

Teodoro Obiang Nguema Mbasogo, 80, ametawala koloni hilo la zamani la Uhispania lenye utajiri mkubwa wa mafuta tangu 1979.

Baada ya kushinda muhula wa sita madarakani mwezi Novemba, waangalizi wa mambo walisema rais alionekana kuwa na shauku ya kukemea madai yanayoendelea, ambayo ameyakanusha.

Hili linaweza kuhatarishwa baada ya Mahakama Kuu ya Uhispania kutangaza kumchunguza mtoto wa kiume wa Obiang, Carmelo Ovono Obiang, mkurugenzi wa usalama wa rais, Isaac Nguema Endo, na waziri wa usalama Nicolas Obama Nchama kwa madai ya kuteka na kutesa.

XS
SM
MD
LG