Upatikanaji viungo

Breaking News
Jumamosi, Aprili 20, 2024 Local time: 14:18

Mtoto wa miaka 13 auawa wakati polisi wakitekeleza amri ya kutotoka nje Kenya


Wasafari wakiwa wamesimama katika mistari inayowatenganisha abiria katika kutekeleza amri ya kutokaribiana ili kuepusha maambukizi ya virusi vya COVID-19 katika kituo cha feri cha Likoni, Mombasa, Kenya. (Photo by - / AFP)
Wasafari wakiwa wamesimama katika mistari inayowatenganisha abiria katika kutekeleza amri ya kutokaribiana ili kuepusha maambukizi ya virusi vya COVID-19 katika kituo cha feri cha Likoni, Mombasa, Kenya. (Photo by - / AFP)

Polisi wameanza uchunguzi kuhusiana na kifo cha mtoto mwenye umri wa miaka 13 aliyekufa baada ya kupigwa risasi akiwa amesimama kwenye varanda ya nyumba yao, jijini Nairobi, Jumatatu.

Mtoto huo alipigwa risasi tumboni polisi walipokuwa wanatekeleza amri ya watu kutotoka nje ya nyumba zao.

Wakati huohuo Rais Uhuru Kenyatta ameomba msamaha kutokana na jinsi maafisa wa polisi walivyotumia nguvu kupita kiasi dhidi ya raia wakati wakitekeleza amri ya kusalia majumbani inapotimia saa moja kamili jioni.

Polisi wameshutumiwa kutumia nguvu kuzidi kiasi wakati wakitekeleza amri hiyo, tangu ilipoanza ijumaa wiki iliyopita.

Wametumia gesi ya kutoa machozi, virungu, fimbo na hata kufatua risasi dhidi ya raia.

XS
SM
MD
LG