Abu Agila Mohammad Masud Kheir Al-Marimi, anashutumiwa kwa uhalifu huo wa mwaka 1988 ambao umetajwa kuwa tukio la kigaidi la kimataifa.
Wizara ya sheria ya Marekani ilitangaza Jumapili kwamba Masud alikuwa amekamatwa, miaka miwili baada ya kufunguliwa mashtaka yanayohusiana na shambulizi hilo.
Maafisa wengine wa ujasusi wa Libya wamefunguliwa mashtaka nchini Marekani kwa kushiriki katika tukio hilo lakini Masud amekuwa wa kwanza kufikishwa katika mahakama ya Marekani kuhusiana na kesi hiyo.
Ndege iliyokuwa inaelekea New York, ililipuka chini ya saa moja baada ya kupaa kutoka London, Desemba 21, 1988. Ilikuwa imebeba raia kutoka nchi 21, waliofariki. Miongoni mwao walikuwa Wamarekani 190.