Upatikanaji viungo

Breaking News
Jumapili, Machi 23, 2025 Local time: 22:59

Mkuu wa zamani katika Jeshi la Burkina Faso ametekwa nyara nyumbani kwake


Ramani ya Burkina Faso na maeneo yaliyo jirani nae.
Ramani ya Burkina Faso na maeneo yaliyo jirani nae.

“Walifunga kitongoji, wakaizingira nyumba yake kabla ya kumchukua,” chanzo kimoja cha cha usalama kimeeleza

Mkuu wa zamani wa wafanyakazi katika jeshi la Burkina Faso ambaye alifutwa kazi mwezi Oktoba ametekwa nyara kutoka nyumbani kwake na “watu wasiojulikana waliokuwa na silaha”, vyanzo karibu naye vimesema Jumatatu.

“Walifunga kitongoji, wakaizingira nyumba yake kabla ya kumchukua,” chanzo cha usalama kilicho karibu na mkuu huyo wa zamani wa polisi kiliiambia AFP. Luteni kanali Evrard Somda alichukuliwa Jumapili kutoka nyumbani kwake katika mji mkuu, Ouagadougou, aliongeza.

“Hatujui kama ni kukamatwa kwa amri ya jeshi au mamlaka ya mahakama, au kama ni utekaji nyara mwingine,” chanzo kingine karibu na Somda kilisema. Somda alifutwa kazi wiki moja baada ya maafisa wanne wa polisi kukamatwa kwa tuhuma za kuhusika katika njama dhidi ya usalama wa taifa ambapo utawala wa kijeshi ulisema ulizuia.

Afisa huyu aliyeheshimika, Somda alikuwa katika wadhifa huo tangu Februari 2022 lakini aliona nafasi yake ikidhoofishwa kutokana na kukamatwa kwa maafisa hao wanne, ambapo walikuwepo washirika wake wawili wa karibu.

Forum

XS
SM
MD
LG