Habari kutoka Libya zinaeleza kwamba mke wa kanali Gaddafi, Safiya, binti yake Ayesha na watoto wa kiume Muhammad na Hannibal waliondoka Libya mapema Jumatatu na kuingia Algeria.
Balozi wa Algeria katika Umoja wa Mataifa amesema walipokelewa kwa misingi ya kibinadamu. Maafisa huko Algiers wanasema waliripoti taarifa hiyo kwa katibu mkuu wa Umoja wa Mataifa na Baraza la mpito la Libya
Viongozi wa upinzani wa Libya wamesema kuwapa hifadhi familia ya Gaddafi ni kitendo cha uchokozi, na wametaka warejeshwe nchini Libya.
Viongozi wa waasi hapo awali wameituhumu Algeria, taifa pekee la Afrika kaskazini ambalo halijatambua Baraza la Mpito la Taifa, kwa kumsaidia Gadhafi na kumpaytia wamamluki ili kukandamiza upinzani wa wananchgi. Algeria imekanusha madai hayo.
Kiongozi wa Libya Gadhafi hadi hivi sasa hajulikani alipo pamoja na vijana wake wengine. Maafisa wqa vyeo vya juu wawaasi walitangaza Jumatatu kwamba huwenda mtoto wa kiume wa Gadhafi, Khamis , mkuu wa kikosi maalum cha wanamgambo wa jeshi ameuliwa katika mapambano siku ya Jumamosi kusini mwa tripoli.