Upatikanaji viungo

Breaking News
Alhamisi, Machi 28, 2024 Local time: 16:02

Mitt Romney ashinda uchaguzi wa kwanza wa Iowa


Matokeo ya uchaguzi wa kwanza wa awali wa wagombea wanane wa chama cha Republican wanaotaka kumondowa madarakani rais Barack Obama, wakati wa uchaguzi mkuu
Matokeo ya uchaguzi wa kwanza wa awali wa wagombea wanane wa chama cha Republican wanaotaka kumondowa madarakani rais Barack Obama, wakati wa uchaguzi mkuu

Romney alishinda kwa kura 8 akifuatwa na Santorum katika uchaguzi wa kwanza wa chama cha republican ulokua na ushindani mkubwa.

Mgombea kiti wa chama cha Republican ambae hakuwa akitajwa sana Rick Santorum, kwa mshangao mkubwa wa wengi amechukua nafasi ya pili katika uchaguzi wa awali wa jimbo la Iowa, nchini Marekani.

Uchaguzi huo ulofanyika Jumanne katika utaratibu wa kumchagua mgombea atakae kiwakilisha chama cha Republican katika uchaguzi mkuu, ulikua na ushindani mkubwa hadi dakika ya mwisho pale Romney aliyekua wakati wote akitarajiwa kupata ushindi alishinda kwa tofauti ya kura nane.

Mgombea mwengine aliyefanya vizuri bila ya kutegemewa ni mbunge Ron Paul aliyetokea watatu na hivyo kubadilisha kabisa mashindano katika chama hicho cha kihafidhina katika kumchagua mgombea atakae pambana na rias Barack Obama katika uchaguzi wa rais baadae mwaka huu.

XS
SM
MD
LG