Upatikanaji viungo

Breaking News
Ijumaa, Aprili 19, 2024 Local time: 22:58

Milipuko miwili yatokea huko Kaduna Nigeria.


Soko lililolipuliwa na Boko Haram huko Kano.
Soko lililolipuliwa na Boko Haram huko Kano.

Milipuko miwili yatokea Kaduna Nigeria lakini idadi ya watu waliojeruhiwa bado haijajulikana.

Mashahidi wanasema milipuko miwili imetokea katika mji wa kati wa Nigeria wa Kaduna Jumanne ikiwa mmoja karibu na kambi ya jeshi.

Polisi walisema mlipuko mmoja ulitokea karibu na daraja na mwingine katika kambi ya jeshi ya kitengo cha ufundi nje kidogo ya Kaduna . Maafisa wanasema idadi ya waliojeruhiwa haijajulikana.

Polisi walikuwa wakichunguza ripoti kwamba mlipuko wa kwenye kambi ya jeshi ulisababishwa na mlipua mabomu wa kujitoa muhanga ambaye aliingiza gari mbele ya eneo la kuingilia.

XS
SM
MD
LG