Akizungumza na shirika la habari la Reuters alisema uhusiano kati ya utawala wa kijeshi nchini Mali na washirika wake wa kimataifa unakaribia kuvunjika baada ya kushindwa kuandaa uchaguzi kufuatia mapinduzi mawili ya kijeshi.
Siku ya Jumatano, utawala huo wa kijeshi uliiambia Ufaransa ikome kuingilia kati masuala ya lililokuwa koloni lake na kukaa na matakwa yao ya kikoloni wao wenyewe.
Waziri wa Mambo ya Nje wa Ufaransa Jean-Yves Le Drian alisema Ijumaa kuwa hali iliyojitokeza haikutegemewa, kwani washirika wa Ulaya walikubali kuandaa mipango ndani ya wiki mbili ya jinsi ya kurekebisha kampeni zao, ambazo zinaijumuisha Mali na eneo kubwa la Sahel, kutokana na hali ya halisi ya mabadiliko.
Masharti ya kuingilia kati kwetu, iwe kijeshi, kiuchumi au kisiasa, yamekuwa magumu zaidi na magumu kuyadhibiti, Parly alisema.
Kwa kifupi, hatuko tayari kulipa gharama isiyo na kikomo ili kubaki nchini Mali.
Lakini alisema mawaziri kutoka nchi 15 zinazohusika na kikosi maalum cha Ulaya kwa sasa wameungana katika kudumisha operesheni hivyo lazima tuamue masharti yake mapya.