Upatikanaji viungo

Breaking News
Jumatatu, Januari 13, 2025 Local time: 12:45

Mashirika ya Kimataifa yatafuta njia mbadala za kupeleka misaada ya Sudan


Malori ya kubeba misaada yakiwa kwenye barabra inayounganisha bandari ya Port Sudan na mji mkuu wa Khartoum.July 10, 2023.
Malori ya kubeba misaada yakiwa kwenye barabra inayounganisha bandari ya Port Sudan na mji mkuu wa Khartoum.July 10, 2023.

Afisa wa ngazi ya juu wa Umoja wa Mataifa amesema Jumatatu kwamba mashirika ya kutoa misaada nchini Sudan yanatafuta njia mpya za upelekaji wa misaada, kupitia Sudan Kusini, wakati mapigano ambayo yamekuwa ykiendelea kwa miezi 9 yakisababisha janga kubwa la kibinadamu nchini humo.

Vita kati ya jeshi la serikali na kundi la kijeshi la Rapid Support Forces, RSF, vimeacha karibu nusu ya wakazi milioni 49 wa Sudan, wakiwa kwenye hali ya kuhitaji misaada. Kwa mujibu wa shirika la habari la Reuters, zaidi ya watu milioni 7.5 wametoroka makwao, na kwa hivyo kufanya taifa hilo kuongoza ulimwenguni katika idadi ya watu waliotoroka makwao.

Kumekuwa na ripoti za misaada kuibwa, pamoja na kushambuliwa kwa wafanyakazi wa misaada, wakati mashirika ya kimataifa ya kutoa misaada yakilalamika kuhusu vizingiti vilivyoko kweye bandari ya Port Sudan, inayodhibitiwa na jeshi, wakati wakijaribu kufikisha misaada kwenye sehemu nyingine za nchi.

Forum

XS
SM
MD
LG