Upatikanaji viungo

Breaking News
Jumatatu, Januari 13, 2025 Local time: 16:17

Marekani yaipinga ICJ kushughulikia mabadiliko ya hali ya hewa


Katika kusikilizwa kwa kesi Jumatano, ndani ya mahakama ya kimataifa ya haki ya The Hague, Marekani imejibu kwamba sheria za haki za binadamu za mataifa hazina mashiko kwa wajibu wa kisheria kwa mabadiliko ya hali ya hewa.

Margaret Taylor, mshauri wa sheria wa wizara ya mambo ya nje anayeiwakilisha Marekani, Jumatano ametoa hoja kwamba mahakama ya ICJ si sehemu sahihi kushughulikia masuala ya haki za masuala ya hali ya hewa.

Amesema idara ya Umoja wa Mataifa ya mabadiliko ya hali ya hewa na mkataba wa Paris ni majukwaa pekee ya kimataifa kisheria ambayo yapo mahsusi yaliyowekwa na mataifa kushughulikia mabadiliko ya hali ya hewa.

Baraza kuu la Umoja wa Mataifa mwaka jana lilitoa mwito kwa mahakama ya ICJ kuzungumzia kisheria kama mataifa yanayo changia kwa kiasi kikubwa mabadiliko ya hali ya hewa yanaweza kuwajibishwa kisheria kwa kusababisha tatizo hilo na madhara inayoleta.

Forum

XS
SM
MD
LG