Upatikanaji viungo

Breaking News
Alhamisi, Aprili 18, 2024 Local time: 09:41

Marekani na washirika wake wajadili njia za kupunguza zaidi mapato ya Russia



Waziri wa fedha wa Canada Chrystia Freeland, waziri wa fedha wa Marekani Janet Yellen, na mawaziri wengine wa fedha wa nchi wanachama wa G7, wakati wa mkutano wa G7, Ujerumani, May 19, 2022. Picha ya Reuters
Waziri wa fedha wa Canada Chrystia Freeland, waziri wa fedha wa Marekani Janet Yellen, na mawaziri wengine wa fedha wa nchi wanachama wa G7, wakati wa mkutano wa G7, Ujerumani, May 19, 2022. Picha ya Reuters

Marekani inafanya mazungumzo na Canada na washirika wengine duniani ili kuzuia zaidi mapato ya nishati ya Moscow kwa kuweka kikomo cha bei ya mafuta ya Russia bila kusababisha athari kwa nchi zenye pato la chini, waziri wa fedha wa Marekani Janet Yellen amesema Jumatatu.

"Tunazungumza juu ya bei ya kikomo au bei maalum ambayo itadumisha na kuimarisha vikwazo vya hivi karibuni vya nishati vilivyopendekezwa na Umoja wa Ulaya, Marekani, Uingereza na wengine, ambayo itateremsha bei ya mafuta ya Russia na kupunguza mapato ya Putin, huku ikiruhusu usambazaji zaidi wa mafuta kufika kwenye soko la kimataifa," Yellen amewambia waandishi wa habari mjini Toronto.

"Tunadhani bei maalum pia ni njia muhimu ya kuzuia madhara mabaya kwa nchi maskini zenye pato la chini ambazo zinataabika kutokana na gharama ya juu ya chakula na nishati," Yellen amesema, akizungumza pamoja na waziri wa fedha wa Canada Chrystia Freeland.

XS
SM
MD
LG