Upatikanaji viungo

Breaking News
Jumatatu, Aprili 28, 2025 Local time: 19:13

Marekani kuendelea kuunga mkono Israel licha ya mabadiliko ya kiutawala


Waziri mkuu mpya wa Israel Benjamin Netanyahu na mke wake Sara Netanyahu baada ua kuchaguliewa tena. Novemba 2, 2022.
Waziri mkuu mpya wa Israel Benjamin Netanyahu na mke wake Sara Netanyahu baada ua kuchaguliewa tena. Novemba 2, 2022.

Waziri wa mambo ya nje wa Marekani Antony Blinken amesema Jumapili kwamba Marekani haitalegeza uungaji mkono wake kwa Israel licha ya tofauti za kisiasa zilizopo na waziri mkuu mpya Benjamin Netanyahu

Tamko hilo limetolea licha ya wasi wasi kutoka kwa utawala wa Biden kuhusu viongozi atakaowachagua kwenye serikali yake yenye msimamo wa mrengo wa kulia.

Wakati akizungumza na kundi lenye msimamo wa mrengo wa kushoto ambalo linalaumiwa kuwaunga mkono wapalestina pamoja na Iran, Blinken amesema kwamba Marekani itabaki kuwa rafiki wa karibu wa Israel.

Hilo litafanyika licha ya kuwa na misimamo tofauti na Ntenyahu kama vile kuundwa kwa mataifa mawili katika kutatua mzozo kati ya Israel na Palestina, pamoja na kurejeshwa kwa mkataba wa nyuklia wa Iran wa 2015.

Ameongeza kusema kwamba ushirikiano uliopo kati ya Marekani na Israel ni thabiti kuliko wakati wowote ule.

XS
SM
MD
LG