Upatikanaji viungo

Breaking News
Alhamisi, Aprili 25, 2024 Local time: 17:04

Mapato kutoka kwa madini yaongezeka DRC


Sehemu ya kuchimba madini ya shaba, Kamoa
Sehemu ya kuchimba madini ya shaba, Kamoa

Mauzo ya madini ya jamhuri ya kidemokrasia ya Congo yameongezeka kwa kiwango kikubwa mwaka 2021 ikilinganishwa na mwaka 2020.

Mapato kutokana na madini ya shaba yameongenzeka kwa asilimia 12.3, tani milioni 1.8 zikiuzwa katika soko la kimataifa.

Mapato kutokana na madini ya Cobalt yameongezeka kwa asilimia 7.4 kutokana na tani 93,011 kuuzwa kwa soko la kimataifa.

Kilo 31,698 za dhahabu zilichimbwa nchini DRC, ikiwa ni ongezeko la asilimia 2.5.

Hesabu hiyo imetolewa na wizara ya madini ya Jamhuri ya kidemokrasia ya Congo.

DRC ni mzalishaji mkubwa wa madini ya shaba na inaongoza kwa usalishaji wa Cobalt kote dunani.

Madini ya Cablt yanatumika kwa kutengeneza betri za magari yanayotumia umeme.

XS
SM
MD
LG