Upatikanaji viungo

Breaking News
Alhamisi, Aprili 25, 2024 Local time: 16:41

Majeshi ya Kenya yapambana kwa mara ya kwanza na al-Shabab


Wanajeshi wa Kenya wakijipanga kutia mafuta kwenye helikopta ya kusafirisha vifaa katika uwanja wa ndege wa Garrisa karibu na mpaka kati ya Kenya na Somalia Oktoba 18, 2011.
Wanajeshi wa Kenya wakijipanga kutia mafuta kwenye helikopta ya kusafirisha vifaa katika uwanja wa ndege wa Garrisa karibu na mpaka kati ya Kenya na Somalia Oktoba 18, 2011.

Msemaji wa jeshi la Kenya Meja Emmanuel Chirchir, anasema wanajeshi wa Kenya walokua wanasonga mbele walipambana na wapiganaji wa al-Shabab Alhamisi na kuwauwa tisa kati yao.

Taarifa za jeshi la Kenya zinasema wanajeshi wake walishambuliwa na wapiganaji 45 wa al-Shabab Alhamis huku majeshi hayo yakisogea karibu na mji wa Al- Qoqani kusini mwa Somalia kudhibiti maeneo yake.

Taarifa hiyo inasema wapiganaji 9 wa al-Shabab wameuawa na wanajeshi wawili wa Kenya kujeruhiwa mmoja wao akiwa katika hali mahtuti. Wanajeshi hao inaripotiwa wamerudishwa Kenya kwa ndege kupata matibabu.

Akizungumza na Sauti ya Amerika msemaji wa jeshi la Kenya Meja Emmanuel Chirchir amesema “mapema asubuhi ya leo tumeweza kutumia ndege zetu kupiga ngome za al-Shabab katika mahala inayoitwa Anole na tukaweza kuvunja kambi yao ya mafunzo na kambi yao ya logistic”.

Wanajeshi wa Kenya wamechukua pia udhibiti wa mji wa Busar wakisogea kuelekea miji mingine miwili ya Burahache na Burgayo. Wanamgambo wa al-Shabab hawajatoa tamko hadi sasa juu ya mapigano ya leo.

Meja Chirchir, anasema mvua kali zinazuia kidogo kampeni yao lakini mambo yanaendelea vyeme na wameweza kusababisha hasara kidogo kwa al-Shabab maeneo ya kusini jambo ambalo wamekuwa wakidhumania kufanya ili kudhibiti maeneo hayo kabla ya wanaharakati kurudi na kuyateka tena kama walivyofanya wakati wa mashambnulizi ya Ethopia.

XS
SM
MD
LG