Upatikanaji viungo

Breaking News
Alhamisi, Machi 27, 2025 Local time: 12:23

Mahakama ya Michigan yakataa kuondoa jina la Trump kwenye orodha ya wagombea urais


Jengo la Mahakama Kuu ya jimbo la Michigan.
Jengo la Mahakama Kuu ya jimbo la Michigan.

Mahakama ya Juu ya jimnbo la Michigan imesema Jumatano kwamba litaendelea kuweka jina la rais wa zamani wa Marekani Donald Trump kwenye orodha ya wagombea kwenye uchaguzi wa mapema.

Mahakama hiyo imesema kwamba haitasikiliza rufaa iliyowasilishwa dhidi ya uamuzi wa mahakama ya chini kutoka kwa makundi yanayoshinikiza jina la Trump liondolewe.

Uamuzi huo ni kufuatia ule wa Desemba 19, uliofanywa na mahakama ya Juu ya Colorado iliyogawanyika, ukisema kwamba Trump hafai kuwania urais kutokana na jukumu lake la Jan 6, 2021, kwenye shambulizi dhidi ya jengo la bunge la Marekani.

Uamuzi huo ulikuwa ni mara ya kwanza katika historia ambapo kifungo cha 3 cha marekebisho ya 14 ya Katiba ya Marekani kimetumika kumuondoa mgombea urais wa Marekani kwenye uchaguzi.

Kesi za Michigan na Colorado ni miongoni mwa darzeni zinazolenga kuondoa jina la Trump kwenye uchaguzi wa majimbo.

Forum

XS
SM
MD
LG