Upatikanaji viungo

Breaking News
Jumamosi, Aprili 20, 2024 Local time: 06:22

Maeneo kadhaa Beijing yamefungwa kutokana na ongezeko la omicron


Wasafiri wakijikinga dhidi ya COVID-19, wakivuka mpaka wa China-Hong Kong kwenye bandari ya Shenzhen, Machi 14, 2022. REUTERS/Tyrone Siu
Wasafiri wakijikinga dhidi ya COVID-19, wakivuka mpaka wa China-Hong Kong kwenye bandari ya Shenzhen, Machi 14, 2022. REUTERS/Tyrone Siu

Mamlaka nchini China zimeripoti visa 1,337 vya ugonjwa wa COVID-19 katika miji kadhaa ya China bara Jumatatu wakati maambukizi yakisambaa kwa  haraka.

Mamlaka nchini China zimeripoti visa 1,337 vya ugonjwa wa COVID-19 katika miji kadhaa ya China bara Jumatatu wakati maambukizi yakisambaa kwa haraka.

Kwa mujibu wa mamlaka hiyo maambukizi hayo yanayojulikana kama stealth Omicron, yakichochea mlipuko mkubwa sana China katika kipindi cha miaka miwili.

Katikati mwa Beijing maeneo kadhaa ya kibiashara na makazi ya watu yamefungwa katika siku za karibuni kutokana na kesi mpya.

Hata hivyo kesi nyingi mpya ziko mbali kaskazini mashariki mwa jimbo la Jilin ambako kuna kesi 895 zilizoripotiwa.

Shenzhen imeripoti kesi mpya 75 wakati wakaazi wanaanza duru ya kwanza kati ya tatu ya vipimo kwa watu wote.

Jumapili maafisa wamefunga mji ambao una wakaazi milioni 17.5 .

XS
SM
MD
LG