Upatikanaji viungo

Breaking News
Jumatatu, Machi 20, 2023 Local time: 18:19

Maelfu ya shule na huduma za jamii zimefungwa Uingereza kutokana na mgomo


Huduma za treni huko Uingereza zinatarajiwa kuzorota kutokana na mgomo unaoendelea huko

Muungano wa vyama vya wafanyakazi, ulikadiria kuwa hadi wafanyakazi nusu milioni, wakiwemo walimu, wafanyakazi wa vyuo vikuu, watumishi wa umma, maofisa wa mipakani na madereva wa treni na mabasi, wataondoka kazini kote nchini

Maelfu ya shule nchini Uingereza zinafunga baadhi au madarasa yao yote, huduma za treni zitazorota na kunatarajiwa kuwepo ucheleweshaji katika viwanja vya ndege Jumatano katika kile kinachoelekea kuwa siku kubwa zaidi ya hatua za viwanda ambazo Uingereza imeshuhudia kwa zaidi ya muongo mmoja, huku vyama vya wafanyakazi vikiongeza shinikizo kwa serikali kudai malipo bora huku kukiwa na mzozo wa gharama za maisha.

Muungano wa vyama vya wafanyakazi, ulikadiria kuwa hadi wafanyakazi nusu milioni, wakiwemo walimu, wafanyakazi wa vyuo vikuu, watumishi wa umma, maofisa wa mipakani na madereva wa treni na mabasi, wataondoka kazini kote nchini.

Hatua zaidi, ikiwa ni pamoja na wauguzi na wafanyakazi wa magari ya kubeba wagonjwa, zimepangwa katika siku na wiki zijazo.

Waingereza wamevumilia miezi kadhaa ya usumbufu katika maisha yao ya kila siku huku mzozo mkali kuhusu malipo na mazingira ya kazi ukiendelea kati ya vyama vya wafanyakazi na serikali. Lakini mgomo wa Jumatano unaashiria kuongezeka kwa hatua za kuvuruga shughuli katika viwanda vingi muhimu.

Mara ya mwisho nchi hiyo kushuhudia matembezi makubwa kwa kiwango hiki ilikuwa mwaka 2011 ambapo zaidi ya wafanyakazi milioni moja wa sekta ya umma walifanya mgomo wa siku moja katika mzozo kuhusu mafao ya wastaafu.

Wakuu wa vyama vya wafanyakazi wanasema licha ya baadhi ya nyongeza ya mishahara kama vile ofa ya asilimia tano ambayo serikali ilipendekeza kwa walimu mishahara katika sekta ya umma imeshindwa kuendana na kupanda kwa kasi ya mfumuko wa bei kwa ufanisi maana wafanyakazi wamekuwa wakipunguziwa mishahara.

Facebook Forum

XS
SM
MD
LG