Upatikanaji viungo

Breaking News
Ijumaa, Machi 28, 2025 Local time: 05:23

Maelfu waandamana Uturuki siku ya Wanawake Duniani


Maelfu ya wanawake waliandamana katika mitaa ya miji ya Uturuki Jumamosi kuadhimisha Siku ya Kimataifa ya Wanawake, kupinga ukosefu wa usawa na unyanyasaji dhidi ya wanawake.

Kwa upande wa Asia wa Istanbul, mkutano wa hadhara wa Kadikoy ulishuhudia washiriki wa vikundi kadhaa vya wanawake wakisikiliza hotuba, kwa kucheza na kuimba.

Maandamano hayo ya kupendeza yalisimamiwa na polisi wengi, wakiwemo askari waliovalia mavazi ya kuzuia ghasia na lori la maji ya kuwasha.

Serikali ya Rais Recep Tayyip Erdogan, ilitangaza 2025 kuwa Mwaka wa Familia. Waandamanaji walipinga wazo la kuamini jukumu la wanawake ni kuwa wake na wazazi tu, wakiwa wamebeba mabango yenye maandishi “Familia haitatufunga kimaisha” na “Hatutatolewa kwa ajili ya familia tu.”

Wakosoaji wameishutumu serikali kwa kusimamia vikwazo vya haki dhidi ya wanawake na kutofanya vya kutosha kukabiliana na unyanyasaji wa wanawake.

Forum

XS
SM
MD
LG