Waandamanaji hao waliokuwa kwenye bustani kuu mjini humo walisikika wakisema kuwa Nikol ni msaliti wakati maafisa wa usalama wakishika doria kwenye ofisi za kiongozi huyo zilizoko karibu.
Kundi lingine linasemekana kuingia kwenye majengo ya serikali na kuzua vurugu huku wengine wakisemekena kufunga barabara kuu. Kiongozi wa muungano wa upinzani wenye vyama zaidi ya darzeni moja ameapa kuitisha maandamano ya kila siku hadi pale Pashinyan atakapo kubali kukabidhi madaraka kwa serikali ya mpito itakayo twikwa jukumu la kuitisha uchaguzi wa bunge ndani ya kipindi cha mwaka mmoja.
Vazgen Manukian ambaye ameidhinishwa na muungano huo kwa jina National Salvation Movement, kuongoza serikali ya mpito ameomba jeshi la Armenia pamoja na polisi kukaidi amri za Pashinyan na kujiunga na watu wengine. Awali Pashinyan aliweka wazi kuwa hakuwa na nia ya kuondoka madarakani.
Imetayarishwa na Harrison Kamau