Upatikanaji viungo

Breaking News
Jumapili, Februari 09, 2025 Local time: 10:30
VOA Direct Packages

Libya yaombwa kuondoa sheria kandamizi ya uhalifu wa kimitandao na Human Rights Watch


Kamisheni ya kitaifa ya haki za binadamu ikiwa imeitisha kikao na wanaharakati wanawake mjini Derna mashariki mwa Libya, (Photo credit: Zahia Faraj Ali)
Kamisheni ya kitaifa ya haki za binadamu ikiwa imeitisha kikao na wanaharakati wanawake mjini Derna mashariki mwa Libya, (Photo credit: Zahia Faraj Ali)

Shirika la Human Rights Watch Jumatatu limeishi  mamlaka mashariki mwa Libya kuifuta  sheria kandamizi ya uhalifu wa mitandao inayowatia hatiani watu wanaojieleza kwa amani pamoja na kuendelea kushikiliwa kwa wale waliokamatwa kutokana na tuhuma hizo.

Kwa mujibu wa shirika la habari la AFP, sheria hiyo iliyopitishwa mwaka jana inadai “kulinda hadhi pamoja na tabia za umma,” bila kufafanua kwa kina.

HRW lenye makao yake mjini New York kupitia taarifa limesema kwamba “ Ni lazima baraza la wawakilishi la Libya litathmini upya sheria ya 2022 ya kupinga uhalifu wa kimitandao, inayominya uhuru wa mazungumzo.

Libya ilitumbukia kwenye ghasia 2011 baada ya kuondolewa kwa dikteta Moamer Kadhafi, na imegawanyika kati ya serikali mbili, moja ikiwa magharibi kwenye mji mkuu wa Tripoli, na nyingine mashariki mwa nchi ikiongozwa na Khalifa Haftar pamoja na baraza la wawakilishi.

XS
SM
MD
LG