Upatikanaji viungo

Breaking News
Jumamosi, Julai 27, 2024 Local time: 04:26

Kura zinahesabiwa Gambia baada ya uchaguzi wa rais


Watu wasubiri kufunguliwa kituo cha kupiga kura katika mtaa wa Manjai Kunda mjini Banjul
Watu wasubiri kufunguliwa kituo cha kupiga kura katika mtaa wa Manjai Kunda mjini Banjul

Vituo vya kupiga kura kwenye uchaguzi wa Gambia vimefungwa na maafisa wa uchaguzi wameanza kuhesabu kura kupitia mfumo wa kipekee wa kuhesabu gololi zilizotumiwa kupiga kura.

Wagambia walijitokeza kwa wingi mkubwa Jumamosi, kulingana na maafisa wa uchaguzi, ili kushiriki kwenye uchaguzi wa kwanza wa kidemokrasia katika muda wa miaka 27 bila ya kuwepo kwa jina la kiongozi wa zamani wa kimabavu Yahya Jammeh.

Uchaguzi huu unafuatiliwa kwa karibu kabisa kwani ni mtihani kwa demokrasia changa ya taifa hilo dogo la Afrika Magharibi.

Upigaji kura nchini humo ni wa kipekee ambapo kila mgombea ana kua na sanduku lake la kura na wapiga kura wanatumbukiza gololi iliyotengenezwa maalum kwa ajili ya uchaguzi.

Maafisa wa uchaguzi wafunga sanduku za kura baada ya upigaji kura kukamilika
Maafisa wa uchaguzi wafunga sanduku za kura baada ya upigaji kura kukamilika

Hii ni kutokana na hali kwamba watu wengi kati ya wakazi milioni 2 wa Gambia hawajui kusoma wale kuandika na hivyo hakuna vyeti vya kupiga kura.

Kiongozi wa kimabavu Jammeh alilazimika kukimbia uhamishoni Equatorial Guinea Januari baada kukataa kushindwa na Adama Barrow hapo Januari 2017.

Ingawa hakuweza kushiriki kwenye uchaguzi huo lakini inaripotiwa amekua na ushawishi mkubwa miongoni mwa wafuasi wake.

Rais Barrow mwenye umri wa miaka 56 anagombania kwa mhula wa pili akikabiliwa na upinzani kutoka wagombea watano akiwemo waziri wake wa zamani wa mambo ya kigeni anaeongoza upande wa upinzani, mwanasiasa mkongwe Ousainou Darboe.

Ousainou Darobe, kiongozi wa upinzani akiwasili kwenye kituo cha kupiga kura
Ousainou Darobe, kiongozi wa upinzani akiwasili kwenye kituo cha kupiga kura

Wagambia ambao kulingana na Benki Kuu ya dunia ndio watu maskini duniani wanataka mabadiliko ya kweli na ya dhati ya kiuchumi. Wengi walompigia kura Barrow kwenye uchaguzi wa 2016 wanasema hawajaridhika na uwongozi wake kwani hajaleta mabadiliko ya kubadili maisha yao.

Vyanzo vya habari hii ni AFP.

XS
SM
MD
LG