Upatikanaji viungo

Breaking News
Alhamisi, Machi 28, 2024 Local time: 14:41

Kundi la ADF ladaiwa kuuwa watu 20 DRC


Familia ikiwalilia ndugu zao waliouawa na kundi la waasi wa ADF huko Beni, Kivu kaskazini, Novemba15 2019. (VOA/Erikas Mwisi)
Familia ikiwalilia ndugu zao waliouawa na kundi la waasi wa ADF huko Beni, Kivu kaskazini, Novemba15 2019. (VOA/Erikas Mwisi)

Watu wanaodhaniwa kuwa wapiganaji wa kundi la waasi la Allied Democratic Forces – ADF, wameuwa zaidi ya watu 20 katika vijiji viwili mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo.

Shambulizi la Alhamisi ni mwendelezo wa mauaji yanayoripotiwa kutekelezwa na makundi ya waasi nchini Congo.

Kulingana na Umoja wa Mataifa, UN, Kundi la waasi la ADF kutoka Uganda, linalofanya mashambulizi ya kila mara mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo kwa zaidi ya miongo mitatu, hadi sasa limeua zaidi ya watu 1,000 tangu mwaka 2019.

UN umehusisha mashambulizi hayo ambayo yameongezeka kwa kiasi kikubwa tangu mwanzoni mwa mwaka huu, na kaunzishwa kwa msako wa jeshi la taifa dhidi ya makundi ya waasi.

XS
SM
MD
LG