Upatikanaji viungo

Breaking News
Jumanne, Aprili 16, 2024 Local time: 20:38

Kizza Besigye akamatwa tena


Jumatatu Kizza Besigye, wa pili kulia, alijikuta katika patashika hii wakati anajaribu kutembea kwa mara nyingine kwenda kazini kwa miguu.
Jumatatu Kizza Besigye, wa pili kulia, alijikuta katika patashika hii wakati anajaribu kutembea kwa mara nyingine kwenda kazini kwa miguu.

Hii ni mara ya tatu katika muda wa wiki mbili kwa Besigye kukamatwa na serikali akitembea kwenda kazini, serikali inasema ni maandamano yasiyo halali.

Kiongozi wa upinzani nchini Uganda Kizza Besigye amekamatwa tena leo - mara ya tatu katika muda wa wiki mbili - akiwa njiani kwenda kazini kwa miguu, hatua ambayo serikali inasema ni njama za kufanya maandamano yasiyo halali.

Besigye na wafuasi wake wamekuwa wakitembea kwa miguu kwenda kazini kila Jumatatu na Alhamisi kupinga ongezeko la bei za mafuta na chakula nchini humo pamoja na matumizi mabaya ya mali ya umma wanayodai kufanywa na serikali ya rais Museveni.

Lakini serikali inasema matembezi hayo ni maandamano yasiyo halali na kwamba itawakamata ambao wanashiriki katika maandamano hayo.

Ripoti nyingine kutoka Kampala zinasema leo kuwa Besigye ameondolewa mjini Kampala na anashikiliwa sehemu nyingine ndani ya nchi hiyo ili kuondoa uwezekano wa wafuasi wake kufanya fujo mjini Kampala

XS
SM
MD
LG