Upatikanaji viungo

Breaking News
Alhamisi, Machi 27, 2025 Local time: 22:42

Kiongozi wa upinzani India adai kufanyiwa zengwe


Kiongozi wa upinzani nchini India, Rahul Gandhi, Jumamosi amesema kuwa ameondolewa bungeni kwa sababu ya kumuuliza Waziri Mkuu Narendra Modi, maswali magumu ya uhusiano wake na Gautam Adani, mwanzilishi wa muungano wa Adani.

Chama cha kihindu cha Modi, Bharatiya Janata kilijibu kwamba Gandhi aliadhibiwa chini ya sheria kwa maoni ya kashfa aliyotoa mnamo 2019 na haikuwa na uhusiano wowote na suala la Adani.

Gandhi, rais wa zamani wa chama kikuu cha upinzani nchini India cha Congress ambaye bado ni kiongozi wake mkuu, alipoteza kiti chake cha ubunge siku ya Ijumaa, siku moja baada ya mahakama ya jimbo la magharibi la Gujarat kumtia hatiani katika kesi ya kashfa na kumhukumu kifungo cha miaka miwili gerezani.

Mahakama ilimpa dhamana na kusitisha kifungo chake kwa siku 30, na kumruhusu kukata rufaa.

XS
SM
MD
LG