Upatikanaji viungo

Breaking News
Jumapili, Aprili 27, 2025 Local time: 03:08

Kiongozi wa Islamic State auwawa mashariki mwa Syria


Picha ya maktaba ya nyumba ya kiongozi wa Islamic State iliyoshambuliwa Mei 1, 2023
Picha ya maktaba ya nyumba ya kiongozi wa Islamic State iliyoshambuliwa Mei 1, 2023

Kamandi ya kijeshi ya Marekani imesema Jumapili kwamba shambulizi la anga la Marekani limemuuwa kiongozi wa kundi la Islamic State mashariki mwa Syria.

Taarifa kutoka kwa kamandi hiyo, CENTCOM, imesema kwamba Usamah al Muhajir aliuwawa kwenye shambulizi la Ijumaa, Kamanda wa CENTCOM Jenerali Michael Erik Kurilla amesema kwamba , “ Tumeweka bayana kwamba tutaendelea na azma yetu ya kuishinda ISIS kote kwenye eneo hilo,” akiongeza kwamba kundi hilo limeendelea kuwa tishio siyo tu kieneo lakini pia kwenye sehemu nyinginezo. Taarifa imeongeza kusema kwamba operesheni dhidi ya ISIS kwa ushirikiano na vikosi nchini Iraq na Syria itaendelea kufanikisha kushindwa kwa kundi hilo.

Forum

XS
SM
MD
LG