Upatikanaji viungo

Breaking News
Jumatatu, Mei 06, 2024 Local time: 00:10

Kiongozi mkuu wa Iran, Ayatollah Ali Khamenei, apongeza vikosi vya jeshi la nchi hiyo


Kiongozi Mkuu wa Iran Ayatollah Khamenei akutana na makamanda wa jeshi la Iran mjini Tehran
Kiongozi Mkuu wa Iran Ayatollah Khamenei akutana na makamanda wa jeshi la Iran mjini Tehran

Kiongozi mkuu wa Iran, Ayatollah Ali Khamenei, alivipongeza vikosi vya jeshi la nchi hiyo kwa mafanikio yao katika matamshi yake ya kwanza hadharani tangu Tehran ilipofanya shambulio kubwa la ndege isiyo na rubani na makombora dhidi ya Israeli wiki iliyopita.

Akikutana na makamanda wakuu wa jeshi la Iran Jumapili, Khamenei alivipongeza vikosi vya jeshi kwa mafanikio yao katika matukio ya hivi karibuni. Alikuwa akizungumzia shambulio la anga la Iran dhidi ya Israel Aprili 13.

Vikosi vya jeshi vilionyesha taswira nzuri ya uwezo na nguvu zao na taswira ya kustaajabisha ya taifa la Iran, Khamenei alisema. Pia zilithibitisha kuibuka kwa nguvu ya azma ya taifa la Iran katika ngazi ya kimataifa, aliongeza.

Forum

XS
SM
MD
LG