Upatikanaji viungo

Breaking News
Jumapili, Machi 23, 2025 Local time: 23:05

Kimbunga Lee kinaelekea pwani ya New England, Marekani na Canada mashariki


Mfanyakazi wa jiji anatazama wimbi linalopiga wakati wa dhoruba Lee, Jumamosi, Septemba 16, 2023 bandari ya Bar Maine. (Picha ya AP/Robert F. Bukaty)
Mfanyakazi wa jiji anatazama wimbi linalopiga wakati wa dhoruba Lee, Jumamosi, Septemba 16, 2023 bandari ya Bar Maine. (Picha ya AP/Robert F. Bukaty)

Kimbunga Lee kinaelekea pwani ya New England nchini Marekani na Canada mashariki kikiwa kimepunguza nguvu na kua dharuba ambayo bado inaweza kusababisha upepo mkali wa kiwango cha kimbunga na mawimbi hatari na kuleta mvua nyingi katika maeneo ya mamilioni ya watu.

Hali mbaya ilitabiriwa Jumamosi katika sehemu za majimbo ya Massachusetts na Maine. Hali ya kimbunga inaweza kukumba majimbo ya Canada ya New Brunswick na Nova Scotia. Huko ndiko dhoruba hiyo inatarajiwa kuwasili baadaye mchana.

Hivi sasa kimbunga cha majira ya joto kimegeuka kuwa dharuba kali.. Hali ya dharura imetangazwa katika majimbo ya Massachusetts na Maine. Shirika la huduma za umeme limeripoti maelfu ya wateja hawana umeme kutoka Maine hadi Nova Scotia Canada.

Forum

XS
SM
MD
LG