Upatikanaji viungo

Breaking News
Jumatatu, Machi 27, 2023 Local time: 15:37
VOA Direct Packages

Kampuni ya BGI ya China yakanusha madai ya Marekani kwamba inahusika kwenye ujasusi


Ofisi za BGI mjini Beijing, China, March 25, 2021.

Kampuni ya BGI ya China, ambayo ni mojawapo ya makampuni makubwa zaidi ulimwenguni kwenye masuala ya genetiki imesema Jumapili kwamba kamwe haiwezi kuhusika kwenye ukiukwaji wa haki za binadamu, baada ya Marekani kudai kwamba kuna hatari ya baadhi ya vitengo vyake kuchangia kwenye ujasusi wa China.

Vitengo vitatu vya BGI ni miongoni mwa makampuni ya China yalioordheshwa wiki iliyopita na Marekani kwamba yanazuia ukaguzi wa kitekonlojia wa Marekani kwa misingi ya kiusalama au haki za binadamu.

Wizara ya biashara ya Marekani imeangazia hatari iliyopo kutoka kwa teknolojia ya BGI katika kuchangia ujasusi wa China. Wanaharakati wa haki za binadamu wanasema kwamba Beijing inajaribu kubuni mtandao wenye taarifa za kijenetiki kutoka kwa waislamu pamoja na makundi mengine ya walio wachache nchini China.

Serikali ya China Ijumaa wiki iliyopita ililalamikia Washington kwa kulenga makampuni yake bila sababu. BGI yenye makao yake makuu kwenye mji wa kusini mwa China wa Shenzhen, imesema kwamba inajishugulisha na huduma za kijamii na kisayansi pekee.

Facebook Forum

XS
SM
MD
LG