VIKOSI vimefanikiwa kuwafukua wachimbaji baada kuchimba umbali wa mita 30 na kuwakaribia.
Juhudi za kuwatafuta watu hawa waliofukiwa zilianza tangu Jumatano chini ya usimamizi wa Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Mkoa, Ofisi ya Madini Kanda ya Ziwa Magharibi ikishirikisha kampuni za migodi GGM na Busolwa.
Mkuu wa Mkoa wa Geita, Meja Jenerali Mstaafu, Ezekiel Kyunga, amewaonya wawekezaji wa migodi mkoani Geita hasa wanaoendesha uchimbaji kuzingatia kanuni za usalama hivyo.