Upatikanaji viungo

Breaking News
Ijumaa, Aprili 19, 2024 Local time: 11:21

Jeshi la DRC latangaza ushindi dhidi ya waasi


Baadhi ya wanajeshi wa jeshi la DRC huko mashariki mwa Congo.
Baadhi ya wanajeshi wa jeshi la DRC huko mashariki mwa Congo.

Jeshi la Jamhuri ya Kidemokrasi ya Kongo - DRC limetangaza kuwa limepata ushindi dhidi ya kundi la waasi wa “Yakutumba Kivu Kusini” huko mashariki mwa Congo.

Kwa mujibu wa jeshi hilo vikosi vyake viliweza kumjeruhi kamanda wa waasi. Jeshi pia limesema limefanikiwa kuchukua silaha za kutosha pamoja na kuwakamata wapiganaji 120.

Wakati huo huo kamanda wa operesheni Kivu Kusini, Yave Philemo amewataka waasi waliobaki wasalimishe silaha zao hasa wale waliopo eneo la Ruzuzu linalopakana na mpaka wa Burundi.

Mwandishi wa VOA, Austere malivika anaripoti kutoka Goma huko Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo-DRC.

please wait

No media source currently available

0:00 0:03:06 0:00

XS
SM
MD
LG