Kwa mujibu wa jeshi hilo vikosi vyake viliweza kumjeruhi kamanda wa waasi. Jeshi pia limesema limefanikiwa kuchukua silaha za kutosha pamoja na kuwakamata wapiganaji 120.
Wakati huo huo kamanda wa operesheni Kivu Kusini, Yave Philemo amewataka waasi waliobaki wasalimishe silaha zao hasa wale waliopo eneo la Ruzuzu linalopakana na mpaka wa Burundi.
Mwandishi wa VOA, Austere malivika anaripoti kutoka Goma huko Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo-DRC.