Upatikanaji viungo

Breaking News
Jumatano, Januari 15, 2025 Local time: 10:01

Jaji wa Hong Kong kuamua iwapo wimbo maarufu wa kuitisha demokrasia utapigwa marufuku


Wanaharakati wa demokrasia wainua simu zao wakiimba wimbo wa, Glory to Hong Kong" wakati wa mkutano kwenye bustani ya Chater Garden mjini Hong Kong. Oct. 26, 2019.
Wanaharakati wa demokrasia wainua simu zao wakiimba wimbo wa, Glory to Hong Kong" wakati wa mkutano kwenye bustani ya Chater Garden mjini Hong Kong. Oct. 26, 2019.

Jaji mmoja wa Hong Kong amesema Ijumaa kwamba atafanya uamuzi wiki ijayo kuhusiana na wimbo uliokuwa maarufu mjini humo wakati wa maandamano ya 2019 ya kuipinga serikali.

Serikali inataka wimbo huo wa kuunga mkono demokrasia uondolewe kwenye internet, na usitumiwe. Wimbo huo kwa jina Glory Hong Kong, kwa bahati mbaya uliwahi kuchezwa kwenye hafla za michezo ya kimataifa, badala ya wimbo wa taifa wa China wa March of the Volunteers.

Wakosoaji wameonya kwamba kuzuiliwa kwa wimbo huo ni mfano mwingine wa kuminywa kwa uhuru ndani ya Hong Kong, ambayo ilikuwa koloni la Uingereza. Hong Kong ilirejeshwa kwenye utawala wa China 1997, na tangu wakati huo China imekuwa ikiipokonya uhuru wake, wakati Beijing ikifanya marekebisho ya kisiasa, pamoja na kuweka sheria kali za usalama wa taifa.

Forum

XS
SM
MD
LG