Upatikanaji viungo

Breaking News
Jumatatu, Aprili 21, 2025 Local time: 23:12

Ivory Coast imefungua mipaka yake tangu kutokea janga la Corona


Rais wa Ivory Coast Alassane Ouattara akiwa na wanajeshi wa nchi hiyo Jan 07, 2023
Rais wa Ivory Coast Alassane Ouattara akiwa na wanajeshi wa nchi hiyo Jan 07, 2023

Ivory Coast imefungua mipaka yake yote, miaka mitatu baada ya kufungwa kutokana na janga la virusi vya Corona.

Baraza la mawaziri limesema kwamba hali ya afya nchini humo sasa ni nzuri na shughuli za uchumi zinaweza kuendelea kama kawaida.

Mipaka hiyo pia imefunguliwa ili kutoa fursa kwa maafisa wa usalama kukabiliana na tatizo la wahamiaji haramu.

Kila mtu anayeingia au kutoka Ivory Coast sasa anatakiwa kupitia mipaka rasmi.

Shirika la habari la ufaransa RFI limeripoti kwamba kumekuwa na ongezeko la wakimbizi wanaoingia Ivory Coast kutoka Burkina Faso, na idadi imefikia 8,700.

Wakimbizi hao wanastahili kupokelewa na kutambuliwa kwenye mipaka rasmi.

XS
SM
MD
LG