Upatikanaji viungo

Breaking News
Jumanne, Machi 19, 2024 Local time: 10:31

Ivanka Trump yupo Afrika kuwahamasisha wanawake kiuchumi


Ivanka Trump
Ivanka Trump

Nchini Ethiopia atakutana na wafanyakazi wanawake katika kiwanda cha kahawa na kutembelea kiwanda cha nguo kinachoongozwa na mwanamke.

Ivanka Tramp binti yake Rais Donald Trump, amewasili Addis Ababa, mji mkuu wa Ethiopia kwa ajili ya mkutano siku ya Jumatatu wa kuwashirikisha na kuwahamasisha kiuchumi wanawake. Mbali na kuhudhuria mkutano huo Ivanka ambae pia ni mshauri wa baba yake atakutana na wafanyakazi wanawake katika kiwanda cha kahawa na kutembelea kiwanda cha nguo kinachoongozwa na mwanamke.

Rais Donald Trump alitia saini hati ya rais ya usalama wa kitaifa mwezi Februari kutambua juhudi za maendeleo na mafanikio ya wanawake ulimwenguni-WGDP. WGDP inaeleza ina matumaini ya kuwafikia wanawake milioni 50 ifikapo 2025 kupitia kazi za serikali ya Marekani na marafiki zake.

Haikufahamika bado kama utata unaomkumba Rais wa Marekani utaibuka wakati wa ziara ya binti yake huko Afrika. Rais amekuwa na maneno makali kuhusu Afrika na wahamiaji wake.

XS
SM
MD
LG