Upatikanaji viungo

Breaking News
Jumamosi, Machi 22, 2025 Local time: 09:17

Israel yafanya mashambulizi ya anga ndani ya Gaza kwa kulenga ngome za Hamas


Moshi mkubwa watanda wakati wa mashambulizi ya anga ya Israel katika mji wa Gaza, Oktoba 12, 2023
Moshi mkubwa watanda wakati wa mashambulizi ya anga ya Israel katika mji wa Gaza, Oktoba 12, 2023

Israel imeendelea kuushambulia Ukanda wa Gaza usiku kucha kwa mashambulizi ya anga, kufuatia onyo kwamba wanajeshi wa Israel wanaweza kushambulia eneo linalotawaliwa na Hamas muda wowote.

Jeshi la Israel liliandika kwenye mtandao wa X “ Wakati wa usiku ndege za kijeshi zilishambulia zaidi ya ngome 100 za Hamas katika Ukanda wa Gaza, na kuharibu mashimo ya handaki, maghala ya silaha na darzeni ya makao makuu ya operesheni zao.”

Hata hivyo, Israel imepanga kuondoka katika mji wa kaskazini wa Kiryat Shmona.

Maafisa wamesema Ijumaa kwamba wakazi wa mji huo watapelekwa kwenye hoteli kwa gharama za serikali.

Mji huo unapatikana karibu na mpaka kati ya Israel na Lebanon na umekuwa ukishambuliwa kwa maroketi na makombora kutoka makundi ya wanamgambo wa Palestina.

Waziri mkuu wa Uingereza Rishi Sunak amesafiri leo kuelekea Misri, ikiwa ziara yake ya hivi karibuni Mashariki ya Kati, wakati mzozo unazidi kupamba moto. Sunak tayari amekutana na viongozi wa Israel na mwanamfamle wa Saudi Arabia Mohammed Bin Salman.

Forum

XS
SM
MD
LG