Upatikanaji viungo

Breaking News
Alhamisi, Machi 28, 2024 Local time: 22:35

Israel inataka Iran kuchukuliwa hatua kutokana na silaha zake za nuclear


Kiwanda cha kutengeneza silaha za nuclear cha Iran. PICHA: AP
Kiwanda cha kutengeneza silaha za nuclear cha Iran. PICHA: AP

Waziri mkuu wa Israel Naftali Bennett, ameishutumu Iran kwa kile alichodai kama kuidanganya jumuiya ya kimataifa kuhusu silaha zake za nuclear, wakati wa kikao na mjumbe wa shirika la umoja mataifa la kufuatilia nguvu za nuclear.

Mkuu wa shirika la kimataifa kuhusu nguvu za nuclear Rafael Grossi, ameitembelea Israel ambayo imekuwa ikiishutumu Iran kwa kutengeneza silaha za nuclear na inaunga mkono kurudia mkataba wa nuclear wa mwaka 2015 kati ya Iran na nchi nyingine zenye nguvu duniani.

Bennett ameelezea wasiwasi kuhusu hatua ya Iran kuendelea kutengeneza nguvu za nuclear huku ikisema uongo kwa jumuiya ya kimataifa na kueneza habari potofu.

Amesisitiza umuhimu kwa jumuiya ya kimataifa kuchukua hatua za haraka dhidi ya Iran kwa kutumia nguvu zote ili kuizuia kuendelea kutengeneza nguvu za nuclear.

Israel inaaminika kuwa nchi pekee yenye silaha za nuclear katika mashariki ya kati lakini haijawahi kusema hadharani kwamba inamiliki silaha hizo.

XS
SM
MD
LG