Upatikanaji viungo

Breaking News
Jumamosi, Aprili 20, 2024 Local time: 11:33

Iran inapinga taarifa ya Ujerumani juu ya vikwazo kwa Iran


Msemaji wa wizara ya mambo ya nje wa Iran, Nasser Kanani akizungumza katika mojawapo ya mikutano mjini Tehran, July 13, 2022.
Msemaji wa wizara ya mambo ya nje wa Iran, Nasser Kanani akizungumza katika mojawapo ya mikutano mjini Tehran, July 13, 2022.

Akizungumza na waandishi wa habari katika mkutano wa Jumatatu, msemaji wa wizara ya mambo ya nje ya Iran Nasser Kanani amesema vikwazo kama hivyo vitakuwa kinyume cha sheria

Wizara ya mambo ya nje ya Iran inasema taarifa kutoka kwa maafisa wa Ujerumani kuhusu uwezekano wa kuwekwa vikwazo dhidi ya Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi la Iran haziwajibiki na hazijengi.

Akizungumza na waandishi wa habari katika mkutano wa Jumatatu, msemaji wa wizara ya mambo ya nje ya Iran Nasser Kanani amesema vikwazo kama hivyo vitakuwa kinyume cha sheria.

Waziri wa mambo ya nje wa Ujerumani Annalena Baerbock amesema Ujerumani na Umoja wa Ulaya zinafikiria kuweka vikwazo dhidi ya IRGC. Alikiambia kituo cha utangazaji cha ARD kwamba kuna fikra zinazoendelea za jinsi ya kuiorodhesha IRGC kama kundi la kigaidi.

Matamshi ya Baerbock yamekuja siku moja baada ya kamanda wa IRGC, Hossein Salami, kuwaonya waandamanaji kutoandamana tena.

Iran imeshuhudia maandamano ya wiki kadhaa tangu kifo cha katikati ya mwezi Septemba akiwa chini ya ulinzi wa polisi, Mahsa Amini mwenye umri wa miaka 22, ambaye alikamatwa na polisi wa maadili wa Iran kwa madai ya kukiuka kanuni kali za mavazi ya Kiislamu kwa wanawake.

XS
SM
MD
LG