Upatikanaji viungo

Breaking News
Jumanne, Aprili 16, 2024 Local time: 15:56

Idadi ya waliofariki na Ebola Uganda yaongezeka


Mwathiriwa wa Ebola anazikwa kwenye makaburi ya Waislamu huko Beni, nchini Kongo, Julai 14, 2019. Mamlaka ya afya katika nchi jirani ya Uganda Jumanne, Septemba 20, 2022 iliripoti kwamba mtu aliyefariki siku moja mapema alipimwa na kukutwa na ugonjwa huo. (Picha ya AP/Jerome )
Mwathiriwa wa Ebola anazikwa kwenye makaburi ya Waislamu huko Beni, nchini Kongo, Julai 14, 2019. Mamlaka ya afya katika nchi jirani ya Uganda Jumanne, Septemba 20, 2022 iliripoti kwamba mtu aliyefariki siku moja mapema alipimwa na kukutwa na ugonjwa huo. (Picha ya AP/Jerome )

Idadi ya waliofariki kutokana na mlipuko wa Ebola nchini Uganda imeongezeka hadi kufikia tisa, wizara ya afya ilisema Ijumaa, wiki mbili baada ya mamlaka kutangaza janga hilo katikati mwa nchi.

Idadi mpya ya wagonjwa iliongezeka kutoka saba, takwimu iliyotolewa Ijumaa ilionyesha.

Mwezi uliopita wizara ya afya ilitangaza kifo cha kwanza katika taifa hilo lisilo na bandari kutokana na virusi hivyo, ambavyo viliripotiwa kwa mara ya kwanza mwaka 2019, na kutangazwa kuzuka katika wilaya ya kati ya Mubende.

Ebola ni homa ya hatari ya virusi ya kuvuja damu iliyopewa jina la mto mmoja katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo ambapo iligunduliwa mwaka 1976.

Maambukizi ya binadamu ni kupitia maji maji ya mwili, dalili kuu zikiwa ni homa, kutapika, kutokwa na damu na kuhara.

Milipuko ni migumu kudhibiti, haswa katika mazingira ya mijini.

Wizara ya afya ilituma ujumbe kwenye Twitter siku ya Jumatatu kwamba idadi ya jumla ya visa vya Ebola vilivyotambuliwa nchini humo vilifikia 43, na karibu watu 900 waliokariniana na wagonjwa walitambuliwa.

Wiki iliyopita Rais Yoweri Museveni alitoa uamuzi wa kutoweka vizuizi ili kudhibiti virusi hivyo, akisema kwamba serikali yake ina uwezo wa kudhibiti mlipuko huu kama tulivyofanya hapo awali.

XS
SM
MD
LG