Upatikanaji viungo

Breaking News
Jumatatu, Aprili 28, 2025 Local time: 17:23
VOA Direct Packages

Idadi ya vifo kutokana na tetemeko la ardhi Syria na Uturuki yapita 36,000


Majengo yalioporoka kutokana na tetemeko kwenye mji wa Hatay, Uturuki. Feb 10.2023.
Majengo yalioporoka kutokana na tetemeko kwenye mji wa Hatay, Uturuki. Feb 10.2023.

Timu za waokozi zimeendeela kutafuta manusura kutoka kwenye vifusi vya majengo yalioporomoka Uturuki na Syria, huku idadi ya vifo ikiendelea kuongezeka kufuatia tetemeko la ardhi la wiki iliyopita.

Zaidi ya vifo 36,000 vimeripotiwa kufikiwa leo, takriban 31, 643 vikitokea Uturuki , huku 4,614 vikiripotiwa Syria. Kwenye mji wa Antakya ambayo kihistoria unajulikana pia kama Antioch nchini Utruruki, hasara iliyopatikana haiwezi kueleleza kwa kuwa kuna majengo yalioporomoka kila mahali. Yale yaliobaki wima yanasemekana kuwa na nyufa, wakati baadhi yakibaki kwenye hali hatari ya kuporomoka.

Serikali imesema kwamba inafanya kila iwezalo, ikizingatiwa kwamba janga hilo limeathiri sehemu yenye ukubwa unaoweza kulinganishwa na Uingereza, na kuathiri takrikban watu milioni 13. Rais wa Uturuki Recep Tayyip Erdogan amesema kwamba atajitahidi kukarabati maeneo yalioharibiwa na tetemeko hilo ndani ya mwaka mmoja.

Hata hivyo matumaini ya kupata manusura zaidi yameendelea kudidimia wakati shughuli za uokozi zikikisiwa kusitishwa hivi karibuni. Vikosi vya ulinzi vya Syria ambavyo vinashikilia maeneo yanayoshikiliwa na waasi nchini vimeambia shirika la habari la BBC kwamba shughuli za uokozi zinakaribia kukamilika. Maelfu ya waokoaji wameripotiwa kutafuta manusura usiku kucha nchini Syria na Uturuki.

XS
SM
MD
LG