Upatikanaji viungo

Breaking News
Ijumaa, Machi 29, 2024 Local time: 11:29

Idadi ya vifo kutokana na mafuriko makubwa Afrika Kusini yafikia 341.


Makontena ya shehena yakikumbwa na mafuriko katika eneo la Durban, April 13, 2022. Picha ya AP.
Makontena ya shehena yakikumbwa na mafuriko katika eneo la Durban, April 13, 2022. Picha ya AP.

Idadi ya vifo kutokana na mafuriko ambayo hayajawahi kutokea nchini Afrika Kusini imeongezeka Alhamisi hadi 341 huku helikopta zikizunguka juu ya mji wa kusini mashariki wa Durban kuwatafuta manusura.

Huku barabara na madaraja vikisombwa na mvua kubwa sana wiki hii, waokoaji walijitahidi kupeleka vifaa katika jiji lote, ambapo baadhi ya wakazi hawana umeme wala maji tangu Jumatatu.

“Kiwango cha uharibifu wa maisha ya watu, miundombinu, na mtandao wa utoaji wa huduma katika jimbo hilo haujawahi kutokea,” amesema Sihle Zikalala, mkuu wa Jimbo la KwaZulu Natal.

“Jumla ya watu 40,723 wameathirika. Cha kuskitisha ni kwamba, vifo 341 vimerekodiwa,” ameuambia mkutano wa waandishi wa habari.

XS
SM
MD
LG