Upatikanaji viungo

Breaking News
Alhamisi, Machi 28, 2024 Local time: 19:18

Wakenya wasomewa mashtaka ICC


Mstari wa mwisho ni waziri wa zamani wa elimu wa Kenya William Ruto , kushoto waziri wa zamani wa viwanda Henry Kosgey na mtangazaji Joshua Sang, kulia, wakiskiliza mashtaka dhidi yao huko The Hague Uholanzi, Aprili 7, 2011
Mstari wa mwisho ni waziri wa zamani wa elimu wa Kenya William Ruto , kushoto waziri wa zamani wa viwanda Henry Kosgey na mtangazaji Joshua Sang, kulia, wakiskiliza mashtaka dhidi yao huko The Hague Uholanzi, Aprili 7, 2011

Watuhumiwa watatu kati ya sita katika ghasia za baada ya uchaguzi Kenya wamefika mahakamani ICC

Wakenya watatu wanaotuhumiwa kwa uchochezi wa ghasia za baada ya uchaguzi mwaka 2007 na 2008 nchini Kenya alhamisi wamefika katika mahakama ya uhalifu ya kimataifa ya uholanzi ambapo septemba mosi ICC imesema itaamua kama wana kesi ya kujibu au hapana.

Waziri wa zamani wa elimu William Ruto , waziri wa viwanda Henry Kosgey na mtangazaji wa Radio Joshua Arap Sang walikuwa katika mahakama – The Hague, kujibu mashtaka dhidi ya uhalifu wa binadamu.

(Video ya ICC PIDS)

Mwendesha mashtaka mkuu wa ICC Luis Moreno-Ocampo aliwatuhumu watuhumiwa wote sita kwa kupanga ghasia zilizosababisha vifo vya watu 1, 300 na kukosesha makazi wengine laki tatu.

Ghasia hizo zilizuka baada ya matokeo ya uchaguzi wa marudio mwaka 2007 kutangazwa. wote rais Mwai Kibaki na na kiongozi wa upinzani Raila Odinga walidai kuwa wameshinda .

XS
SM
MD
LG