Shirika hilo limeongeza kusema kwamba mbweha mmoja miongoni mwa watatu waliopatikana wakiwa wamekufa kwenye mbuga ya wanyama ya Meaux, alifanyiwa majaribio kwenye maabara na kudhibitishwa kuwa na homa hiyo.
Shirika la afya duniani ,WHO, mwezi uliopita lilieleza wasiwasi wake kutokana na kuongezeka kwa maambukizi hayo miongoni mwa ndege na wanyama, wakati likitadhmini hatari zake ulimwenguni, zikiwemo kesi za maambukizi ya binadamu hivi karibuni nchini Cambodia.
Homa ya Avian maarufu bird flu imekuwa ikienea kote ulimwenguni katika mwaka mmoja uliopita, na kuuwa zaidi ya ndege milioni 200. Homa hiyo inasemekana kuambukiza paka mmoja nchini Ufaransa Decemba iliyopita.
Facebook Forum