Upatikanaji viungo

Breaking News
Ijumaa, Machi 28, 2025 Local time: 18:16

Hali ya usalama ya Darfur yaendelea kuwa hatarishi -UN yasema


Wakimbizi walioathiriwa na mapigano ya Darfur wakielekea Chad kutafuta hifadhi. Picha ya Reuters. Agosti 4, 2023.
Wakimbizi walioathiriwa na mapigano ya Darfur wakielekea Chad kutafuta hifadhi. Picha ya Reuters. Agosti 4, 2023.

Shirika la kibinadamu la Umoja wa Mataifa, OCHA, limeonya kwamba hali ya wakazi wa eneo la Darfur la Sudan ni hatarishi, wakati mapigano kati ya makundi mawili hasimu ya kijeshi yakiendelea

Hilo ni pamoja na kuongezeka kwa taharuki za kikabila. OCHA limesema kwamba mapigano mapya kati ya jeshi la Sudan na kundi la kijeshi la Rapid Support Forces, RPF, kwenye pande zote za Darfur, yameuwa darzeni ya watu pamoja na kuharibu mali zao.

Ripoti zimeongeza kusema kwamba takriban watu 17 wameuwawa huku 35 wakijeruhiwa katika wiki moja iliyopita huko Nyala, kusini mwa Darfur, wakati wengine 17,500 wakilazimika kutoroka makwao.

Mapigano ya kijeshi pamoja na ya kikabila pia yameripotiwa Kaskazini na Kati mwa Drafur, ambapo watu zaidi wameuwawa, huku wengine wakifurushwa makwao. Msemaji wa OCHA Jens Laerke ameongeza kuwa watu wa Darfur wameteseka kwa muda mrefu na hasa wanawake kwenye mapigano ya miaka ya nyuma na yanayoendelea sasa hivi.

Forum

XS
SM
MD
LG