Watu wa Serbia wanaoishi Kosovo waliandamana mitaani kuwazuia mameya wa Albania, kuingia ofisini.
Makabiliano yalitokea baada ya polisi wa Kosovo kujaribu kuwaondoa waandamanaji ili kuwaruhusu wanasiasa hao kuingia ofisini.
Maafisa wamesema kwamba polisi watano wamejeruhiwa katika makabiliano hayo ya Ijumaa na magari kadhaa kuchomwa moto.
Uingereza, Ufaransa, Italy, Ujerumani na Marekani zimetoaa taarifa ya pamoja kuitaka Kosovo kumalizaa uhasama huo.
Rais wa Serbia Aleksandar Vucic amesema kwamba watalinda amani lakini Serbia haitakaa kimya pale ikiwa kutokea mashambulizi dhidi ya raia wa Serbia wanaoishi kaskazini mwa Kosovo.
Forum