Upatikanaji viungo

Breaking News
Alhamisi, Machi 28, 2024 Local time: 20:46

Hakuna kilichoamuliwa hadi kura zote  zihesabiwe-Lapid


Waziri Mkuu wa Israel na Kiongozi wa chama cha Yesh Atid Yair Lapid akiwahutubia wafuasi wake kutoka jukwaani kwenye makao makuu ya chama chake wakati wa uchaguzi mkuu wa Israel huko Tel Aviv, Israel, Novemba 2, 2022. REUTERS/Amir Cohen
Waziri Mkuu wa Israel na Kiongozi wa chama cha Yesh Atid Yair Lapid akiwahutubia wafuasi wake kutoka jukwaani kwenye makao makuu ya chama chake wakati wa uchaguzi mkuu wa Israel huko Tel Aviv, Israel, Novemba 2, 2022. REUTERS/Amir Cohen

Waziri Mkuu wa zamani wa Israeli Benjamin Netanyahu alionekana yuko katika nafasi nzuri ya kurejea madarakani baada ya maoni katika upigaji  kura kwenye uchaguzi wa Jumanne ambao  ulionyesha kambi yake ya mrengo wa kulia ikielekea kwa wingi wa kura.

Hii ni kutokana na kujitokeza kwa wingi kwa washirika wake wa siasa kali za mrengo wa kulia.

Waziri Mkuu aliyekaa madarakani kwa muda mrefu zaidi wa Israel, akiwa amehukumiwa kwa tuhuma za ufisadi ambazo anakanusha, alikuwa tayari kuchukua viti 61 hadi 62 katika bunge la Knesset yenye viti 120, kulingana na kura za maoni za televisheni ya Israel.

Kura za kutoka maoni zinaweza kutofautiana na matokeo ya mwisho ya uchaguzi, ambayo hayatarajiwi hadi baadaye katika wiki hii. Lakini matokeo yalionyesha kujitokeza kwa wingi kwa upande wa mrengo wa kulia, ambao ulionekana kupungukiwa na wingi.

Waziri Mkuu wa Israel Yair Lapid alisema ni mapema mno kufanya hitimisho kuhusu matokeo ya uchaguzi wa Jumanne kufuatia matokeo ya kura za maoni zenye matumaini kwa mpinzani wake, waziri mkuu wa zamani Benjamin Netanyahu.

Hakuna kilichoamuliwa hadi kura zote zihesabiwe, alisema Lapid, na kuongeza "Tutasubiri kwa subira kwa matokeo ya mwisho."

XS
SM
MD
LG