Upatikanaji viungo

Breaking News
Ijumaa, Machi 29, 2024 Local time: 11:26

Guterres kukutana na Putin kumuomba asitishe uvamizi dhidi ya Ukraine


Katibu mkuu wa Umoja wa mataifa Antonio Guterres akizungumza wakati wa mkutano wa Baraza la usalama la Umoja wa mataifa juu ya mzozo wa Ukraine, April 5, 2022. Picha ya AP
Katibu mkuu wa Umoja wa mataifa Antonio Guterres akizungumza wakati wa mkutano wa Baraza la usalama la Umoja wa mataifa juu ya mzozo wa Ukraine, April 5, 2022. Picha ya AP

Katibu mkuu wa Umoja wa mataifa Antonio Guteress anaelekea mjini Moscow ambapo anatarajiwa kukatana leo Jumanne na Rais wa Russia Vladimir Putin katika jitihada za kumuomba akubali kusitisha au kumaliza kabisa uvamizi wa nchi yake dhidi ya Ukraine ambao umedumu sasa miezi miwili.

Msemaji wa Guterres amesema mkuu huyo wa Umoja wa mataifa atazuru baadaye siku ya Alhamisi mjini Kyiv kukutana na Rais wa Ukraine Volodymyr Zelensky, kwa sababu Guteress anaamini kuna “ fursa halisi” ya kupiga hatua.

Akiwa njiani kuelekea Moscow, Guterres alikutana Jumatatu mjini Ankara na Rais wa Uturuki Recep Tayyip Erdogan, ambaye alijaribu bila mafanikio kuwapatanisha, na kumaliza vita kati ya majirani hao wawili wanaoshirikiana bahari na Uturuki.

Guterres ametoa wito mara kadhaa wa kusitisha mapigano kwa ajili ya shughuli za kibinadamu au kusitisha mapigano kwa muda, lakini bila mafanikio.

XS
SM
MD
LG