Upatikanaji viungo

Breaking News
Jumanne, Desemba 05, 2023 Local time: 18:22

Ghasia zaanza tena kaskazini mwa Nigeria.


Haya ni baadhi ya majengo yalioungua kutokana na mashambulizi ya Boko Haram huko Kano.
Haya ni baadhi ya majengo yalioungua kutokana na mashambulizi ya Boko Haram huko Kano.

Mashambulizi mawili huko Kano kwenye kituo cha Polisi na Maiduguri kwenye soko yanaaminika kuwa ni kundi la Boko Haram limehusika .

Ghasia zimeanza tena kaskazini mwa Nigeria Jumatatu wakati watu wenye silaha wanaoaminika kuwa wanachama wa kundi la kiislam la Boko Haram kushambulia kituo cha Polisi huko Kano.

Mkuu wa Polisi wa eneo hilo Ibrahim Idris alithibitisha shambulio hilo lakini hakutoa taarifa zaidi.

Shambulio jingine lilitokea Jumatatu huko Maiduguri mashariki mwa Kano, ambapo soko lilishambuliwa. Hakukuwa na ripoti za vifo au majeruhi katika mashambulizi hayo mawili.

XS
SM
MD
LG