Upatikanaji viungo

Breaking News
Alhamisi, Aprili 18, 2024 Local time: 12:04

Emmanuel Macron atarajiwa kushinda muhula wa pili


Wafuasi wa Macron wakisherehekea .
Wafuasi wa Macron wakisherehekea .

Rais wa Ufaransa Emmanuel Macron alikuwa kwenye nafasi nzuri  Jumapili ya kushinda muhula wa pili kwa kumshinda kiongozi wa siasa kali za mrengo wa kulia Marine Le Pen katika uchaguzi wa rais, makadirio yalionyesha.

Macron alitazamiwa kushinda kwa asilimia 57.0-58.5 ya kura ikilinganishwa na Le Pen aliyepata asilimia 41.5-43.0, kulingana na makadirio ya makampuni ya ukusanyaji maoni ya vituo vya televisheni vya Ufaransa kulingana na sampuli ya hesabu ya kura.

Matokeo ni madogo kuliko mchuano wao wa duru ya pili mwaka 2017, wakati wagombea hao wawili walikutana katika duru ya pili na Macron alipata zaidi ya asilimia 66 ya kura.

Kiwango kizuri cha ushindi hata hivyo kitampa Macron kujiamini anapoelekea katika muhula wa pili ya miaka mitano, lakini uchaguzi huo pia umewakilisha kwa jinsi gani mrengo wa kulia umekaribia kutaka kushinda mamlaka nchini Ufaransa.

XS
SM
MD
LG