Picha za wafungwa waliokuwa wamenyolewa vichwa, kuchorwa tattoo mwilini, wakiwa bila viatu na wamevaa kaptura nyeupe, zilionyeshwa kwenye mitandao wakati wa zoezi hilo.
Rais wa El Salvador Nayib Bukele ametangaza vita dhidi ya magenge ya wahalifu kwenye taifa hilo la Amerika ya Kati, wakati jela hiyo mpya ikiwa sehemu ya kampeni yake.
Kupitia ujumbe wa Twitter, kiongozi huyo, akielezea kuhusu wafungwa hao amesema, “ haya ndiyo makao yenu mapya na wala hamtaweza kuwadhuru watu tena.”
Hata hivyo makundi ya kutetea haki za binadamu yamepinga kampeni hiyo yakisema kwamba watu wasio na hatia huenda wakalengwa, huku baadhi wakifa hata kabla ya kupata nafasi ya kujitetea. Licha ya hilo, wakazi wengi wa El Salvador wamekaribisha kampeni hiyo.
Facebook Forum