Upatikanaji viungo

Breaking News
Alhamisi, Januari 16, 2025 Local time: 18:57

Dunia yaadhimisha siku ya ukimwi


Watoto wadogo wakitembea kutoka shule moja nchini kenya inayohudumia watoto yatima walioachwa na wazazi wao kutokana na ukimwi.
Watoto wadogo wakitembea kutoka shule moja nchini kenya inayohudumia watoto yatima walioachwa na wazazi wao kutokana na ukimwi.

Shirika la afya duniani linaadhimisha siku ya Ukimwi duniani Jumanne kwa kusisitiza umuhimu wa kuongeza matibabu ya antiretroviral kwa wale wote wanaoishi na virusi vya HIV

Desemba Mosi ni maadhimisho rasmi ya siku ya ukimwi duniani. Mataifa mbalimbali yametoa wito wa kukabiliana na ugonjwa huu na hatimaye kuhakikisha unatokomezwa kabisa.

Nchini tanzania mkurugenzi wa shirika linaloshughulika na afya ya mama na mtoto CSI, Stella Mpanda ametoa wito kwa kina mama ambao ndio waathirika wakubwa kuhakikisha wanazingatia afya zao ili wasiambukizwe.

Siku ya ukimwi duniani
please wait

No media source currently available

0:00 0:04:45 0:00
Kiungo cha moja kwa moja

Wakati huo huo Shirika la afya duniani linaadhimisha siku ya Ukimwi duniani Jumanne kwa kusisitiza umuhimu wa kuongeza matibabu ya antiretroviral kwa wale wote wanaoishi na virusi vya HIV.

Shirika hilo la Umoja wa Mataifa linasema kiasi cha watu milioni 16 kati ya milioni 37 wanaoishi na HIV, vijidudu vinavyosababisha UKIMWI wanatumia mchanganyiko wa dawa ya ARV na kwamba matumizi ya wale wote wanaoishi na vijidudu hivyo ndio njia pekee yanayoweza kutokomeza janga hilo katika kipindi cha kizazi kimoja.

WHO imekariri uchunguzi mbali mbali unaonyesha kwamba wale ambao wanaanza matibabu mara moja baada ya kuambukizwa ni mara chache sana kuambukiza wengine huku wao wakiishi na afya nzuri.

XS
SM
MD
LG